Kampuni ya mafuta ya Msumbiji yakana kumwaga mafuta baharini

0


 Kampuni ya kusambaza mafuta inayomilikiwa na serikali ya Msumbiji, Petromoc, imekanusha kuhusika na umwagaji wa mafuta ulitokea mwishoni mwa wiki katika bandari ya Pemba, karibu na pwani ya mkoa wa Cabo Delgado.

Mwenyekiti wa bodi ya kampuni hiyo Hélder Chambisse amesema kuna maelezo finyu kuhusu chanzo cha mafuta hayo yaliyomwagika bahari.

Alisema laiti kampuni hiyo ilihusika mamlaka katika eneo hilo ingeliwaarifu.

Bw. Chambisse amesema uchunguzi unaendelea kufahamu kilichosababisha umwagikaji huo.

Inakadiriwa kwamba umwagikaji huo umesababisha hasara ya karibu lita 10,000 za mafuta.

Kisa hicho kimevutia umati mkubwa wa watu wakiwemo wanawake na watoto, ambao wanahatarisha maisha yao kuchota mafuta kwenye mitungi.

Polisi wamepelekwa eneo hilo kudhibiti watu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

About Us

Light Speed Template is Designed Theme for Giving Enhanced look Various Features are available Which is designed in User friendly to handle by Piki Developers. Simple and elegant themes for making it more comfortable